Nchi wanachama wa Brics zinakutana nchini Afrika Kusini
Nairobi – Wanachama wa nchi zinazounda muungano wa mataifa ya Brics ikiwemo China, Urusi na India wanakutana nchini Afrika Kusini.
Imechapishwa:
Mkutano huo unafanyika wakati huu nchi wanachama zikiwa zinawazia kuongeza idadi ya wanachama wake kama vile mataifa ya Iran na Argentina.
Wahusika kwa muungano huu wanaouna kama mbadala wa ubabe wa nchi za Magharibi katika taasisi za kidunia.
🇷🇺 His Excellency Foreign Affairs Minister Sergey Lavrov of the Russian Federation arriving in South Africa for the XV BRICS Summit.
— Presidency | South Africa 🇿🇦 (@PresidencyZA) August 22, 2023
His Excellency President Vladimir Putin will join the proceedings virtually. #BRICSZA #BRICS2023 #BetterAfricaBetterWorld 🌍 pic.twitter.com/kMQJ4aW2Kc
Tayari zaidi ya mataifa mapya 20 yameomba kujiunga na muungano huo mpya.
Rais wa Urusi Vladimir Putin, ambaye anakabiliwa na kibali cha kukamatwa kutoka katika mahakama ya uhalifu wa kivita ICC, hatahuduhuria kikao hicho binafsi kama ilivyotarajiwa.
Viongozi kadhaa akiwemo rais wa China Xi Jiping, waziri wa mambo ya kigeni wa Urusi Sergei Lavrov wanahudhuria mkutano huo wa awamu ya 15.
Rais Xi alikaribishwa na mwenyeji wake rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa.
Today’s #ChinaStateVisit takes place within the context of celebrating 25 years of diplomatic relations between the two countries, while historic ties date back to the Bandung conference of 1955. #ChinaInSA 🇨🇳🇿🇦 pic.twitter.com/mlAjvRgUTi
— Presidency | South Africa 🇿🇦 (@PresidencyZA) August 22, 2023
Mapema siku ya Jumapili, rais Ramaphosa alisema Afrika Kusini haitalazimishwa kuegemea nchi zozote katika Nyanja ya kimataifa.
Jumla ya mataifa 69 yamealikwa katika mkutano huo yakiwemo yale ya Afrika.