Pata taarifa kuu

Hali ya utulivu yaanza kushuhudiwa Amhara Ethiopia

Jimbo la Amhara nchini Ethiopia, limeanza kushuhudia utulivu wakaazi wakisema ni kutokana na jeshi la taifa kuwazidi nguvu wapiganaji wa eneo hilo na  kuchukuwa udhibiti wa baadhi ya miji baada ya mapigano ya siku kadhaa.

Mapigano yamekuwa yakishuhudiwa katika eneo hilo kati ya jeshi la serikali na wapiganaji wa Fano
Mapigano yamekuwa yakishuhudiwa katika eneo hilo kati ya jeshi la serikali na wapiganaji wa Fano © AFP
Matangazo ya kibiashara

Idara ya hali ya dharura nchini humo imesema jeshi la taifa limefanikiwa kukomboa jimbo la Amhara baada ya watu wenye silaha inaowaita magaidi kuzidiwa nguvu.

Ni taarifa ambayo pia wafanyakazi wa kutoa misaada eneo hilo wamesema miji mingi ambayo imekuwa ikikaliwa na wapiganaji sasa inathibitiwa na wanajeshi wa serikali, licha ya kwamba bado baadhi  inakaliwa na wapiganaji hao wa Fano.

Hakuna taarifa rasmi iliotolewa na mamlaka za Ethiopia kuhusu hali  ya eneo la Amhara ila madaktari eneo hilo wamekiri kupokea miili ya raia kadhaa ambao wameuawa kutokana na makabiliano kati ya jeshi wa wapiganaji wa Fano.

Serikali ya Ethiopia jumatano ilitangaza hali ya dharura katika jimbo hilo la Amhara ambalo limekuwa lishuhudia utovu wa usalama.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.