Pata taarifa kuu

Nigeria: Rais Tinubu amemfuta kazi mkuu wa tume ya kupambana na rushwa

NAIROBI – Rais mpya wa Nigeria Bola Tinubu amemsimamisha kazi kwa muda usiojulikana mkuu wa Tume ya  kupambana na rushwa nchini humo, Tume ya Uhalifu wa Kiuchumi na Kifedha (EFCC).

Bola Ahmed Tinubu, Rais wa Nigeria
Bola Ahmed Tinubu, Rais wa Nigeria REUTERS - STRINGER
Matangazo ya kibiashara

Abdulrasheed Bawa alitakiwa kuondoka katika wadhifa huo  ili kuruhusu uchunguzi sahihi kuhusu harakati zake wakati  akiwa madarakani".

Ingawa ni jambo la kawaida kwa mkuu wa shirika la kupambana na ufisadi kuondolewa mara tu rais mpya anapoingia madarakani, taarifa ya serikali ilisema kusimamishwa huko kulifuatia tuhuma nzito kuhusiana na  matumizi mabaya ya ofisi yanayomkabili.

Afisa huyo mwenye umri wa 43 amekuwa akikabiliwa na tuhuma za ufisadi  tangu alipoteuliwa kuwa mwenyekiti wa EFCC mnamo 2021, jambo ambalo amekanusha.

Katika mahojiano na BBC Hausa mwezi uliopita, gavana wa zamani wa jimbo la kaskazini la Zamfara alimshutumu  Bawa kwa madai ya kudai hongo ya $2m (£1.58m) kutoka kwake. Alikanusha madai hayo.

Nigeria imeorodheshwa katika nafasi ya 150 kati ya nchi 180 katika mtizamo wa shirika la Transparency International kuhusu ufisadi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.