Pata taarifa kuu

Burkina Faso: Daktari wa Australia aachiliwa miaka 7 baada ya kutekwa nyara

Daktari wa Australia mwenye umri wa miaka 88, Kenneth Elliott, ameachiliwa miaka saba baada ya kutekwa nyara na wanajihadi nchini Burkina Faso, serikali ya Australia imetangaza Ijumaa.

Daktari wa Australia Arthur Kenneth Elliott katika video kutoka tovuti ya  Intelligence Group, shirika linalojulikana kwa kusambaza jumbe za video kutoka kwa mashirika ya kigaidi ya Kiislamu kwa vyombo vya habari vya kimataifa. Julai 2, 2017.
Daktari wa Australia Arthur Kenneth Elliott katika video kutoka tovuti ya Intelligence Group, shirika linalojulikana kwa kusambaza jumbe za video kutoka kwa mashirika ya kigaidi ya Kiislamu kwa vyombo vya habari vya kimataifa. Julai 2, 2017. AFP - -
Matangazo ya kibiashara

Kenneth Elliott na mkewe walitekwa nyara na wanajihadi wenye uhusiano na Al-Qaeda mnamo Januari 2016. Mkewe Jocelyn aliachiliwa mwezi uliofuata.

Daktari huyo wa upasuaji alirejea Australia Alhamisi jioni, Waziri wa Mambo ya Nje wa Australia Penny Wong amewaambia waandishi wa habari.

“Daktari Elliott yuko salama na ameungana tena na mkewe Jocelyn na watoto wao,” Bi Wong amesema.

"Nina furaha kubwa kwamba kuachiliwa kwake kumepatikana na kwamba yuko salama tena na familia yake," ameongeza.

Kutekwa nyara kwa wanandoa hao kulidaiwa na kundi la wanajihadi la Ansar Dine, linalohusishwa na Al-Qaeda.

Mnamo Julai 2017, shirika la Al-Qaeda huko Maghreb (Aqmi) lilirusha video inayoonyesha mateka sita, akiwemo Kenneth Elliott.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.