Pata taarifa kuu

Sudan: Jeshi na RSF zakubaliana kuwalinda raia wakati huu mapigano yakiendelea

NAIROBI – Jeshi na wanamgambo wa RSF nchini Sudan, wametia saini mkataba wa kuheshimu hali ya kibinadamu wakati huu mapigano yakiendelea lakini wameshindwa kukubaliana kuhusu kusitisha vita.

Jeshi na wapiganaji wa RSF nchini Sudan wamekubaliana kuwalinda raia wakati mapigano yakiendelea
Jeshi na wapiganaji wa RSF nchini Sudan wamekubaliana kuwalinda raia wakati mapigano yakiendelea AFP - -
Matangazo ya kibiashara

Pande hizo mbili zimekubaliana kuwalinda raia na kuweka mbele maslahi yao mbele, kwa mujibu wa mkataba huo, uliotiwa saini na wawakilishi wa kiongozi wa kijeshi Abdel Fattah al-Burhan na kiongozi wa kundi la RSF Mohamed Hamdan Daglo.

Makubaliano hayo, yanamaanisha kuwa pande hizo mbili, zitawaruhusu raia kukimbilia katika maeneo salama, watakayochagua.

Mapigano ya pande mbili za kijeshi nchini Sudan yamesababisha mamia ya raia nchini humo kukimbia makazi yao
Mapigano ya pande mbili za kijeshi nchini Sudan yamesababisha mamia ya raia nchini humo kukimbia makazi yao AP - Donaig Le Du

Hii imekuja baada ya wawakilishi hao kuendelea na mazungumzo yanayoendelea jijini Jeddah, chini ya uangalizi wa Saudi Arabia na Marekani.

Licha ya kutiwa saini kwa mkataba huo, ripoti zinasema, makubaliano hayo hayajaanza kuheshimiwa, wakati huu mapigani yakiendelea jijini Khartoum.

Wapatanishi wa mzozo wa Sudan wanataka kusitsihwa kwa mapigano kuruhusu utoaji wa misaada kuwafikia walioathirika
Wapatanishi wa mzozo wa Sudan wanataka kusitsihwa kwa mapigano kuruhusu utoaji wa misaada kuwafikia walioathirika REUTERS - RULA ROUHANA

Wajumbe wa Marekani kwenye mazungumzo hayo, wanasema mambo bado ni magumu, lakini hatua ya kukubaliana kuheshili hali ya kibinadamu ni muhimu.

Kwa karibu mwezi mmoja sasa, vita vinavyoendelea vimesababisha vifo vya watu 750 na kuwaacha wengine zaidia ya Elfu tano, wakiwa na majeraha na Laki tisa kukimbia makaazi yao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.