Pata taarifa kuu

Zambia: Rais Hichilema aagiza kuuzwa kwa magari yaliyonunuliwa kabla hajaingia madarakani

NAIROBI – Rais Hakainde Hichilema wa Zambia amemuagiza Katibu wa baraza la mawaziri Patrick Kangwa kuhakikisha kuwa magari yote ya kifahari yaliyonunuliwa kwa ajili ya maofisa wakuu wa serikali wakati wa utawala wa UPND yanauzwa.

Hakainde Hichilema, rais wa Zambia
Hakainde Hichilema, rais wa Zambia REUTERS - SHELLEY CHRISTIANS
Matangazo ya kibiashara

Rais alibainisha kuwa utawala wake uliapa kuzuia ubadhirifu miongoni mwa maafisa wa serikali, jambo ambalo lilidhihirika katika utawala uliopita. Kwa hiyo, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia kiapo hicho, akieleza zaidi kuwa magari hayo ya kifahari hayana ulazima.

Alisisitiza dhamira ya serikali yake ya kuwatumikia watu wa Zambia na kuhakikisha uwajibikaji kutoka kwa maofisa walioteuliwa.

Rais Hichilema alielezea kusikitishwa kwake na baadhi ya mawaziri na makatibu wakuu kushindwa kutekeleza majukumu yao na badala yake walikuwa na shughuli nyingi za kuvinjari mtandaoni.

Alitoa changamoto kwa watendaji wakuu serikalini kuwajibika kwa wapiga kura ambao licha ya kukabiliwa na mazingira magumu bado waliwapigia kura.

Maagizo ya rais ni sehemu ya juhudi za utawala wake kupunguza matumizi ya serikali na kudhibiti ufisadi.

Amesisitiza mara kwa mara hitaji la maofisa walioteuliwa kutekeleza majukumu yao ili kuhakikisha utekelezaji mzuri wa sera na programu za serikali yake.

Uuzaji wa magari ya kifahari yaliyonunuliwa hapo awali kwa maafisa wakuu wa serikali unatarajiwa kuongeza mapato kwa serikali huku pia ikiashiria dhamira ya utawala ya kupunguza gharama zisizo za lazima.

Umma umepongeza uamuzi wa rais, huku wengi wakiuita kuwa ni hatua sahihi kuelekea utawala bora.

Agizo la rais la kuuza magari ya kifahari yaliyonunuliwa kwa ajili ya maafisa wakuu wa serikali wakati wa utawala wa UPND ni ishara ya kujitolea kwa utawala wake katika uwajibikaji na kupunguza matumizi ya serikali.

Hatua hiyo huenda ikakaribishwa na umma na kudhihirisha zaidi dhamira ya rais ya kutekeleza sera na mipango ya serikali yake ipasavyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.