Pata taarifa kuu

Sudan: Usitishaji mapigano wa saa 72 unaingia siku ya mwisho leo Alhamisi

NAIROBI – Nchini Sudan, usitishaji mapigano wa saa 72 ulioafikiwa kufuatia juhudi za Marekani unaingia katika siku yake ya tatu na ya mwisho Alhamisi hii.

Wanajeshi maalum wa RSF nchini Sudan wanakabiliana na wale wa serikali
Wanajeshi maalum wa RSF nchini Sudan wanakabiliana na wale wa serikali AFP - -
Matangazo ya kibiashara

Licha ya hilo makubaliano hayo hayajaheshimiwa kikamilifu licha ya kushuhudiwa kwa utulivu katika baadhi ya maeneo, huku maeneo mengine mapigano kati ya vikosi vya jenerali Al Burhan na Emeti yakiendelea. Wakati huu jeshi likisema liko tayari kuongeza muda wa usitishwaji wa mapigano.

Katika siku ya tatu ya usitishaji mapigano, makabiliano yameendelea kushuhudiwa katika mji mkuu wa Sudan ambapo ndege za kivita za jeshi ziliruka katika vitongoji vya kaskazini, zikishutumiwa kurusha mizinga mikubwa kuelekea katika ngome za wanamgambo.

Wanajeshi wa serikali ya Sudan wamekuwa wakikabiliana na vikosi vya RSF
Wanajeshi wa serikali ya Sudan wamekuwa wakikabiliana na vikosi vya RSF AFP - EBRAHIM HAMID
Viunga vya mashariki mwa Khartoum vilikumbwa na mashambulio makali ya anga na mapigano ya bunduki yalifanyika katika viunga vya kusini, ambapo kunapatikana makaazi ya jenerali Emeti.

Mashuhuda wanasema jiji la Kharthum limeshuhudia utulivu kwa muda mfupi kifuatia makubaliano, ambapo hata hivyo makubaliano hayo yalivunjwa mara moja na kuanza kushuhudiwa kwa mara nyingine tena ubabe katika ya pande mbili zinazokinzana.

Maelfu ya raia wa Sudan wametoroka nchini humo kufuatia mapigano kati ya vikosi viwili vya jeshi.
Maelfu ya raia wa Sudan wametoroka nchini humo kufuatia mapigano kati ya vikosi viwili vya jeshi. AFP - AMER HILABI
Tangu kuanza kwa mapigano hayo April 15, kati ya wababe wawili wa kijeshi jenerali Alburhan na naibu wake jenerali Hemedti, kumezuka pia sakata la wafungwa kutoroka katika jela mbalimbali nchini humo ambapo jana jumatano jeshi lililazimika kutoa msimamo juu ya kiongozi wa zamani wa nchi hiyo Omar el Bashir  anaetafutwa na mahakama ya uhalifu wa kivita ya ICC.

Omar el-Béchir , rais wa zamani wa Sudan
Omar el-Béchir , rais wa zamani wa Sudan REUTERS - Mohamed Nureldin Abdallah
Magenge pia yamekuwa yakipora nyumba na majengo matupu, yakilenga magari anaongeza. Wenyeji wanahofia kitakachotokea baada ya kumalizika kwa usitishaji mapigano.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.