Pata taarifa kuu

Hali ilivyo nchini Sudan kufikia leo Jumanne

NAIROBI – Pande zinazopigana nchini Sudan, zimekubaliana kuhusu hatua ya kusitishwa kwa makabiliano katika kipindi cha saa 72, hatua inayokuja wakati huu mataifa ya Magahribi, nchi za kiarabu na Asia yakiwemo mataifa mengine ya Afrika yakiendelea kuwaondoa raia wake nchini humo.

Raia wa kigeni wamendelea kuondolewa nchini Sudan wakati huu pia mapigano yakiwa yamesitishwa kwa saa 72
Raia wa kigeni wamendelea kuondolewa nchini Sudan wakati huu pia mapigano yakiwa yamesitishwa kwa saa 72 REUTERS - EL TAYEB SIDDIG
Matangazo ya kibiashara

Licha ya makubaliano hayo, kumeripotiwa kuzuka kwa makabiliano katika eneo la Geneina Magharibi mwa jimbo la Darfur kati ya wanajeshi wa Sudan na wanajeshi maalum wa RSF.

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Antonio Guterres ameonya kuwa mapigano yanyoendelea nchini humo yanaweza kuathiri mataifa jirani na taifa hilo.

Katibu mkuu wa UN ametoa wito wa kusitishwa kwa mapigano nchini Sudan
Katibu mkuu wa UN ametoa wito wa kusitishwa kwa mapigano nchini Sudan AP - SALVATORE DI NOLFI
Wizara ya mambo ya kigeni ya Misiri imesema mfanyikazi wake ameuawa katika mapigano hayo katika mji wa Khartoum wakati akiwa katika shughuli zake za kikazi.

Raia na majeruhi

Karibia watu zaidi ya 427 wamethibitishwa kufariki katika mapigano hayo wakati wengine zaidi ya 3,700 wakiwa wamejeruhiwa kwa mujibu wa ripoti ya umoja wa mataifa.

Makumi kwa maelfu ya watu, wakiwemo raia wa Sudan na raia wa kigeni, wamekimbilia nchini Misri, Chad na Sudan Kusini katika siku chache zilizopita.

Raia wa Kigeni wanaendelea kuondolewa jijini Khartoum wakati huu mapigano yakiendelea
Raia wa Kigeni wanaendelea kuondolewa jijini Khartoum wakati huu mapigano yakiendelea © El-Tayeb Siddig / Reuters
Marekani na mataifa ya Ulaya, Mashariki ya Kati, Afrika na Asia yalianzisha misheni ya dharura ili kuwaweka salama wafanyakazi wa ubalozi wao na raia wa Sudan kwa njia za barabara, anga na baharini.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, kuna uhaba mkubwa wa chakula, maji safi, dawa na mafuta na uhaba wa mawasiliano na umeme. Bei za bidhaa hizo pia zikiripotiwa kupanda.

Diplomasia

Jeshi la Sudan na RSF wamekubaliana kusitisha mapigano kwa saa 72 baada ya kufanyika kwa mazungumzo ya kina, Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken alisema muda mfupi kabla ya kutekelezwa kwa makubaliano hayo kuanzia saa sita usiku wa kuamkia leo Jumanne.

"Usitishaji huu wa mapigano unalenga kuruhusu raia na wakaazi kupata rasilimali muhimu, huduma za afya, na maeneo salama, huku pia wakiwaondoa raia wa kigeni kwa kuzingatia kidiplomasia," RSF iliandika kwenye Twitter.

Blinken alisema Marekani itaratibu na maslahi ya kiraia ya kikanda, kimataifa na Sudan kuunda kamati ya kusimamia kazi ya usitishaji vita wa kudumu na mipango ya kibinadamu.

Antony Blinken, Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani
Antony Blinken, Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani REUTERS - ELIZABETH FRANTZ
Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, Josep Borrell, alisema zaidi ya raia 1,000 wa Umoja wa Ulaya wamehamishwa kwa kutumia safari za ndege za Ufaransa, Ujerumani na nchi zingine.

Baraza la usalama la umoja wa mataifa linapanga mkutano kuhusu Sudan siku ya Jumanne.

Mataifa kadhaa - ikiwa ni pamoja na Kanada, Ufaransa, Poland, Uswizi na Marekani - yamesitisha shughuli katika balozi zake katika kipindi cha muda usiojulikana.

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa aliwataka wanachama 15 wa baraza la usalama kutumia nguvu zao kuirejesha Sudan katika njia ya mpito ya kidemokrasia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.