Pata taarifa kuu

Mapigano nchini Sudan yanaingia wiki ya pili hali ikiendelea kuwa mbaya

NAIROBI – Nchini Sudan licha ya wito wa Kimataifa wa kusitishwa kwa mapigano wakati wa sikukuu ya Eid Fitr, jeshi la taifa na wanamgambo wa RSF wameendelea kupigana, jijini Khartoum na maeneo mengine ya nchi, na kusababisha idadi ya watu waliopoteza maisha kuongezeka.

Mapigano yanaendelea kurindima nchini Sudan licha ya wito wa kusitishwa
Mapigano yanaendelea kurindima nchini Sudan licha ya wito wa kusitishwa AFP - -
Matangazo ya kibiashara

Wakaazi wa Khartoum wamelazimika kusalia katika makaazi yao huku wengine wakiendelea kutorokea maeneo salama, huku jeshi na kundi la RSF likipambana kwa risasi na mabomu.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guteress na Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani, Anthiny Blinken walikuwa wametoa wito kwa pande zote kusitisha vita angalau kwa siku tatu katika kipindi hiki cha EID lakini wito wao umepuuzwa.

Antonio Guterres, katibu mkuu wa umoja wa mataifa ametoa wito wa kusitishwa kwa makabiliano nchini Sudan
Antonio Guterres, katibu mkuu wa umoja wa mataifa ametoa wito wa kusitishwa kwa makabiliano nchini Sudan REUTERS - AHMED SAAD
Wanamgambo wa RSF nao walisema walikuwa tayari kusitisha vita kwa saa 72 kuanzia Ijumaa asubuhi, lakini wakaazi wa Khartoum na maeneo mengine wameripoti kuendelea kusikia milio ya risasi na milipuko.

Huku makabiliano yakiendelea, Shirika ma afya duniani limetoa takwimu mpya, zinazoonesha kuwa, idadi ya watu waliopteza masiha katika mapigan hayo, imeongezeka na kufikia zaidi ya 400 huku wengine zaidi ya Elfu tatu wakijeruhiwa.

Maelfu ya raia wa Sudan wameendelea kutoroka katika mji mkuu wa Khartoum wakihofiwa kushambuliwa
Maelfu ya raia wa Sudan wameendelea kutoroka katika mji mkuu wa Khartoum wakihofiwa kushambuliwa REUTERS - EL TAYEB SIDDIG

Miongoni mwa waliopoteza maisha ni mfanyakazi wa Tume ya Umoja wa Mataifa inayohusika na wahamiaji IOM, ambaye imeelezwa aliuawa baada ya kushambuliwa wakati akielekea katika mji wa Kusini wa El Obeid.

Jeshi linasema kuwa limetuma silaha zaidi na wanajeshi katika  barabara za mji wa Khartoum kuwatafuta wanachama wa Kikosi pinzani cha Wanajeshi wa Rapid Support Forces RSF.

Mapigano yamesababisha uharibifu mkubwa wa mali nchini Sudan
Mapigano yamesababisha uharibifu mkubwa wa mali nchini Sudan © AFP
Mgogoro huo ulisababisha waumini wengi wa dhehebu ya kiislamu kusalia nyumbani wakati wa siku kuu ya Eid, kinyume na miaka ya nyuma kwani wengi waliohofia usalama wao. Misikiti mingi mjini Khartoum na Omdurman zikifungwa.

Mapingano hayo yameshuhudia vituo vingi vya matibabu vikiathiriwa na kukosa vifaa vya kutosha vya kutibu. Pamoja na Khartoum, eneo la magharibi la Darfur, pia limeathiriwa vibaya na mapigano.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.