Pata taarifa kuu

Makabiliano yanaendelea nchini Sudan, mataifa ya kigeni yakiwaondoa raia wake

NAIROBI – Mapigano yameingia wiki ya pili leo nchini Sudan, kati ya wanajeshi wa serikali na wanamgambo wa RSF, ambayo yamesababisha watu zaidi ya 400 kupoteza maisha na maelfu kujeruhiwa.

Moshi ukifuka kwenye majengo ya makazi mashariki mwa Khartoum mnamo Aprili 22, 2023, wakati wa mapigano yanayoendelea kati ya vikosi vya majenerali wawili wanaoshindana.
Moshi ukifuka kwenye majengo ya makazi mashariki mwa Khartoum mnamo Aprili 22, 2023, wakati wa mapigano yanayoendelea kati ya vikosi vya majenerali wawili wanaoshindana. AFP - -
Matangazo ya kibiashara

Wakaazi wa Khartoum, wameendelea kusikia, milio ya risasi na milipuko, baada ya utulivu wa muda mfupi kushuhudiwa hapo jana, siku ya kwanza ya Sikukuu ya Eid.

Licha ya pande zote kukubali kuacha mapigani wakati wa sikukuu ya Eid, wakabiliano yameendelea, huku jeshi la Sudan likitangaza kuwa limekubali kusaidia mipango ya kuwaondoa nchini humo raia wa kigeni.

Makabiliano yanayendelea nchini Sudan kati ya wanajeshi na vikosi maalum vya RSF
Makabiliano yanayendelea nchini Sudan kati ya wanajeshi na vikosi maalum vya RSF AFP - -
Mataifa ya kigeni kama Marekani, Uingereza, Ufaransa na China yamekuwa yakionesha nia ya kutaka kuwaondoa raia wake waliokwama jijiji Khartoum.

Saudi Arabia imekuwa nchi ya kwanza kufanikiwa kuwaondoa raioa wake 50 baada ya kutumia usafiri wa boti ambao wamewasili kwenye mji wa bandari wa Jeddah.

Wachambuzi wa mizozo kutoka Shirika la International Crisis Group,  wanaonya kuwa iwapo suluhu ya haraka haitapatikana, huenda ukasambaa na kuwa wa kikanda.

Haya yanajiri wakati huu jeshi la Sudan likisema kuwa wanadiplomasia na raia kutoka katika nchi za Marekani, Uingereza, Ufaransa na China wataondolewa nchini humo  kwa ndege wakati huu huku mapigano yakiendelea kati ya wanajeshi wa serikali na vikosi maalum vya RSF.

Maelfu ya raia wa Sudan wanaendelea kuondoka nchini humo wakiwemo raia wa kigeni
Maelfu ya raia wa Sudan wanaendelea kuondoka nchini humo wakiwemo raia wa kigeni AFP - -
Taarifa kutoka kwa jeshi imesema raia wa Uingereza, Marekani, Ufaransa na China na wanadiplomasia wataondolewa kwa ndege kwenye ndege za usafiri wa kijeshi kutoka mji mkuu, Khartoum.

Saudi Arabia pia imetangaza kuwa inapanga kuwahamisha raia wa Saudia na raia wa nchi "ndugu" kutoka Sudan.

Jeshi la Sudan limesema kuwa tume ya kidiplomasia ya Saudi Arabia tayari imeondolewa. Mgogoro huo umeingia wiki yake ya pili licha ya pande zote mbili - jeshi na RSF kukubaliana kusitisha mapigano kwa siku tatu kuadhimisha sikukuu ya Waislamu ya Eid al-Fitr.

Wakuu wa kijeshi nchini Sudan ambao vikosi vyao vinaendelea kukabiliana
Wakuu wa kijeshi nchini Sudan ambao vikosi vyao vinaendelea kukabiliana AFP - ASHRAF SHAZLY
Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Khartoum umefungwa kutokana na ghasia hizo, huku balozi za kigeni ikiwa ni pamoja na Marekani na Uingereza zimeshindwa kuwarudisha raia wao nyumbani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.