Sitalegeza Kamba dhidi ya wanaokwepa kulipa ushuru: Rais Ruto
Rais wa Kenya, William Ruto, amesisitiza Serikali yake kutolegeza Kamba katika vita dhidi ya watu na makampuni yanayokwepa kulipa kodi, kauli ambayo hata hivyo imetafsiriwa kuwa inawalenga wapinzani wake.
Imechapishwa:
Cheza - 00:35
Kwa majuma kadhaa sasa, rais Ruto, amekuwa akirushiana maneno kuhusu kodi na wapinzani Wake, akidai suala la ulipaji kodi halitaangalia hadhi au nafasi ya mtu aliyonayo kwa jamii.
“Na mimi nimefurahi sana kwamba sasa Kenya yote tumeunganisha mawazo yetu na tumekubaliana hakuna mkubwa wala mdogo mbele ya sheria na sisi wote tutalipa ushuru kulinagana na mapato yetu.”amesema rais Ruto.
Katika hatua nyingine, kinara wa upinzani Raila Odinga, amemkosoa Ruto kwa kile alichosema anajificha nyuma ya suala la ulipaji kodi ili kuficha utepetevu mdogo wa utendaji wa Serikali yake.