Pata taarifa kuu
TANZANIA- SIASA

Tundu Lisu kurejea Tanzania Jumatano wiki hii

Nchini Tanzania, mikutano ya kisiasa, ilirejelewa tena mwishoni mwa wiki iliyopita, kwa chama kikuu cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, kuanza kampeni zake katika ukanda wa Kaskazini kuanzia mjini Mwanza.

Mwanasiasa wa upinzani wa Tanzania Tundu Lisu akiweka saini yake katika Kitabu alichozindua jijini Nairobi Kenya Juni 25 2021
Mwanasiasa wa upinzani wa Tanzania Tundu Lisu akiweka saini yake katika Kitabu alichozindua jijini Nairobi Kenya Juni 25 2021 © RFI Kiswahili-Hilary Ingaty
Matangazo ya kibiashara

Mikutano hii imeanza wakati huu, mwanasiasa wa upinzani Tundu Lissu ambaye amekuwa akiishi uhamishoni, akitarajiwa kurejea nyumbani, siku ya Jumatano, akitokea nchini Ubelgiji alikokuwa anaishi kwa miaka saba.

Musa Lutege ni mchambuzi wa siasa akiwa jijini Dar es salaam.

“Rais wa nchi yetu ameleta mageuzi makubwa ya siasa kupanua demokraisa ambayo ilikuwa imepitia kwenye kipindi cha giza.”amesema Musa Lutege.

Mikutano ya kisiasa ilianza nchini Tanzania, baada ya rais Samia Suluhu Hassan, kutangaza kuondoa marufuku iliyokuwa imewekwa kuzuia mikutano ya hadhara, iliyotangazwa na aliyekuwa rais Hayati John Magufuli.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.