Pata taarifa kuu
KENYA- SIASA

Ruto: Kulikuwepo njama ya kumteka mwenyekiti wa uchaguzi

Nchini Kenya, rais William Ruto, amedai kuwa, kulikuwa na mpango wa kumteka na kumuua, Mwenyekiti wa uchaguzi Wafula Chebukati, ili kubadilisha matokeo ya uchaguzi wa urais, wakati wa uchaguzi mkuu, mwaka uliopita.

Wafula Chebukati aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini Kenya na rais  William Ruto
Wafula Chebukati aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini Kenya na rais William Ruto AFP - TONY KARUMBA
Matangazo ya kibiashara

Ruto ametoa madai hayo katika kikao na Makamishena wa Tume huru, akiwemo Chebukati ambaye muda wake kama Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi umefika mwisho.

“Tunafahamu kwamba kulikuwepo na njama ya kumteka na kumuua Chebukati.” Ameeleza rais Ruto.

Madai haya ya Ruto, yamelaaniwa na wanasiasa wa upinzani, wanaosema ni shutuma zisizokuwa na ushahidi wowote.

Muungano wa Azimio la Umoja, umeendelea kusisitiza kuwa waliibiwa kura katika uchaguzi huo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.