Kenya: Muda wa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi wakamilika
Msikilizaji nchini Kenya, hivi leo ndio muda wa mwisho kuwa madarakani kwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Wafula Chebukati, pamoja na makamishna wengine wawili kati ya 7, hatua ambayo inaacha pengo la uongozi kwenye tume hiyo.
Imechapishwa:
Cheza - 01:13
Ni miaka sita ambayo haikuwa rahisi kwa tume hiyo hasa katika uchaguzi wa mwaka 2017 na ule wa Agosti mwaka jana.
Wanasheria wanamtazamo gani? Carol Korir, amezungumzwa na Steve Oguttu, mtaalamu wa masuala ya utawala akiwa Kenya.
βNafasi ya mwenyekiti ambaye muda wake umekamilika itatangazwa ili watu watume maombi ya kujaza nafasi yake.β amesema Steve Oguttu.
Chebukati amekuwa akituhumiwa na kiongozi wa upinzani Raila Odinga kwa kuhujumu matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita, rais Ruto akimsifia mwenyekiti wa kutangaza matokeo kulinagana na walivyopiga kura raia wa kenya.