WHO yaonya kuhusu mlipuko wa Kipindupindu
Shirika la afya duniani WHO, limeonya kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu unaoendelea kuripotiwa kwenye mataifa zaidi, huku Malawi, Syria na Lebanon, yakitajwa kuathirika zaidi.
Imechapishwa:
Cheza - 00:34
Mkurugenzi wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus, sasa anazitaka nchi kuchukua tahadhari, akihofia athari zaidi kutokana na uhaba wa chanjo za ugonjwa huo.
“Tangu mwezi Januari mwaka jana mataifa 31 ikiwa ni asilimia 50 zaidi ya miaka iliyopita.”Ameeleza Tedros Adhanom Ghebreyesus.
Aidha WHO pia imetoa wito kwa mataifa ya dunia kuwasisitizia raia wake kuvalia barakoa haswa wanaposafiri safari za muda mrefu ilikabiliana na msaambao wa uviko 19 aina ya Omicron.