GUINEA-SIASA
kesi ya mauaji dhidi ya kiongozi wa zamani wa Guinea imeanza tena
Baada ya mapumziko ya wiki tatu, kesi ya mauaji ya Septemba 28, 2009 dhidi ya kiongozi wa zamani wa Guinea, Moussa Dadis Camara na washtakiwa wengine, ilianza tena hapo jana ambapo Camara ameendelea kukanusha tuhuma dhidi yake.
Imechapishwa:
Cheza - 00:26
Matangazo ya kibiashara
Hata hivyo mmoja wa raia wanaofuatilia kwa ukaribu kesi hiyo na ambaye hakutaka jina lake kutajwa amekuwa na kauli hii.
“Mtu ambaye hajulikani ametokea wapi kama kwa bahati tu hivi kapewa madaraka nchini hana uzoefu hajuwi anachokisema yeye mwenyewe.”amesema raia ambaye hakutaka jina lake litajwe.
Inaarifiwa kuwa watu zaidi ya 157 waliuawa na wanawake mia moja kubakwa.