Waziri mkuu wa mpito wa Chad ajizulu
Waziri Mkuu wa Chad amejiuzulu Jumanne, siku moja baada ya tangazo la Jenerali Mahamat Idriss Déby Itno, kuongeza miaka miwili kama rais wa kipindi cha "mpito", na amesema uteuzi ujao wa "serikali ya umoja wa kitaifa", alitangaza N' Djamena.
Imechapishwa:
Albert Pahimi Padacé aliwasilisha barua ya kujiuzulu kwake kwa serikali yake wakati wa mazunguzo na mkuu wa nchi, ambaye alikubali kuachia ngai, kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari kutoka ikulu ya rais. Aliteuliwa miezi 18 iliyopita na Mahamat Déby.
Jumatatu, rais huyo alitawazwa, kwa kipindi kipya cha miaka miwili ya mpito kuelekea "uchaguzi huru na wa kidemokrasia", ambao alikuwa ameahidi miezi 18 iliyopita.
Mnamo Aprili 20, 2021, jeshi la kijeshi la majenerali 15 lilimpeleka hadi mkuu wa nchi hii kubwa ya Sahelia siku moja baada ya kifo cha baba yake Idriss Déby Itno, aliyeuawa mbele ya waasi baada ya kutawala kwa miaka 30 bila kupingwa.