Pata taarifa kuu

Senegal kuendelea kutoa mchango wake wa kijeshi nchini Mali

 Jeshi la Senegal limesema litaendelea kuhudumu katika jeshi la kulinda amani katika nchi jirani ya Mali, baada ya kiongozi wa upinzani kutaka jeshi hilo kurudi nyumbani. 

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakishika doria katika mitaa ya Timbuktu, Julai 13, 2013.
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakishika doria katika mitaa ya Timbuktu, Julai 13, 2013. AP - Rebecca Blackwell
Matangazo ya kibiashara

Katika taarifa yake, jeshi limekanusha ripoti kuwa, linapanga kuondoa vikosi vyake vinavyokadiriwa kuwa zaidi ya 1300 nchini Mali, na kusisitiza kuwa kinachofanyika, ni mzunguko wa kawaida. 

Senegal ambayo inachangia idadi kubwa katika jeshi ma MINUSMA nchini Mali, imeendelea kuwa miongoni mwa wanajeshi wa kigeni wanaosaidia nchi hiyo kupambana na makundi ya kijihadi.  

Ousmane Sonko, mwanasiasa wa upinzani na mkosoaji mkubwa wa rais Macky Sall, amemtuhumu rais wa nchi hiyo kwa kutuma wanajeshi hao katika nchi hiyo jirani kwa sababu ya shinikizo kutoka kwa Ufaransa. 

Sonko ambaye amesema atawania urais mwaka 2024, anasema iwapo ataingia madarakani, atatuma jeshi la nchi yake kushirikiana na lile la Mali kupambana na wanajihadi na kuliondoa kwenye MINUSMA. 

Hii imekuja baada ya Ufaransa kuondoa kabisa wanajeshi wake nchini humo, baada ya kutofautiana  na uongozi wa kijeshi. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.