Pata taarifa kuu
KENYA- SIASA

Kenya: Hatutazima Facebook wakati wa uchaguzi: Waziri Joe Mucheru

Waziri wa masuala ya mawasiliano na teknolijia nchini Kenya, Joe Mucheru, ametupilia mbali uwezekano wa kuufungia mtandao wakijamii wa facebook wakati wa uchaguzi mkuu wa Agosti 9.

Nebo ya  mitandao tofauti za kijami
Nebo ya mitandao tofauti za kijami © Pixabay
Matangazo ya kibiashara

Matamshi yake yanakinzana na yale yaliyotolewa na tume ya maridhiano na utangamano, ambayo ilisema inatoa siku 7 kuanzia jana kwa kampuni ya facebook kudhibiti lugha za uchochezi na chuki zinazochapishwa kwenye mtandao wake.

Waziri Mucheru hata hivyo anasema serikali imejipanga kuhakikisha uhuru wa watu kutoa maoni unaheshimiwa na kwamba haitajihusisha na kutoa vitisho vya kuufungia mtandao huo.

Kauli yake ikijaribu kuzima hofu iliyokuwepo miongoni mwa washika dau kuwa, Serikali inapanga kuzima huduma ya mitandao ya kijamii wakati wa uchaguzi wa Agosti 9, akisisitiza kutofungiwa kwa mtandao wowote wala huduma ya Internet.

Kwa mujibu wa tume ya utangamano na maridhiano, mtandao wa Facebook umeshindwa kuchuja arafa za chuki na uchochezi, hali inayotishia kusababisha vurugu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.