Pata taarifa kuu
ULAYA- AFRIKA -UHUSIANO

Ziara za viongozi wa mataifa ya Ufaransa ,Marekani na Urusi barani Afrika

Viongozi kutoka nchi za Ufaransa, Marekani na Urusi wanazuru bara la Afrika, katika kile kinachoelezwa ni kuyashawishi mataifa ya Afrika kuunga msimamo yao kuhusu vita vinavyoendelea nchini Ukraine.

Rais wa Benin  Patrice Talon  na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron
Rais wa Benin Patrice Talon na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron AFP - LUDOVIC MARIN
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii pia inaelezwa kama ushindani mkubwa wa mataifa hayo kuwahi kushuhudiwa barani Afrika, tangu wakati wa vita baridi.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amekuwa katika nchi za Cameroon, Benin na Guinea Bissau huku akiishtumu Urusi kama mkoloni anayesalia duniani kuwakosoa pia viongozi wa mataifa ya Afrika kutoonesha msimamo thabiti wa kusimama na Ukraine na kuilaani Urusi kwa uvamizi unaoendelea.

Aidha, ameishutumu Urusi kwa kutumia vyombo vyake vya Habari kwa kueneza Habari za propaganda kuhusu vita vnavyoendelea nchini Ukraine.

Naye, Waziri wa Mambo ya nje wa Urusi Sergey Lavrov ambaye amekuwa nchini Misri, Congo Brazavile, Uganda na Ethiopia na kuyashtumu mataifa ya Magharibi kwa kuchochea mzozo kati yake na Ukraine, huku akiitetea nchi yake dhidi ya shutuma za kusababisha kupanda kwa gharama ya vyakula duniani.

Samantha Power, Mkuu wa Shirika la  Kimataifa la Maendeleo nchini Marekani naye alikuwa nchini Kenya na Somalia wiki iliyopita, na sasa balozi wake kwenye Umoja wa Mataifa Linda Thomas-Greenfield, anatarajiwa kuzuru Ghana na Uganda wiki ijayo, katika kile kinachoelezwa ni kuendeleza ushawishi kwa mataifa ya Afrika.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.