Pata taarifa kuu
TUNISIA- SIASA

Tunisia imepitisha katiba mpya, inayompa rais madaraka makubwa

Tunisia imepitisha katiba mpya, inayompa madaraka makubwa rais, baada ya kufanyika kwa kura ya maoni siku ya Jumatatu, ambayo idadi ndogo ya wapiga kura walijitokeza.

Rais wa Tunisia Kais Saied akiwa jijini Tunis na wafuasi wake Julai  26  2022.
Rais wa Tunisia Kais Saied akiwa jijini Tunis na wafuasi wake Julai 26 2022. © AFP PHOTO / HO / TUNISIAN PRESIDENCY PRESS SERVICE
Matangazo ya kibiashara

Licha ya idadi ndogo ya wapiga kura ambayo ni asilimia 30, kujitokeza kushiriki kwenye zoewi hilo, waliunga mkono mabadiliko ya katiba kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi.

Wapinzani nchini humo waliosusia, zoezi hilo wamepinga ushindi huo na kusema matokeo yaliyotangazwa ni ya uongo na kilichotokea, kinarudisha nyuma hatua za demokrasia zilizopigwa.

Hata hivyo, rais Kais Saied, ameongoza wafuasi wake kusherehekea mabadiliko hayo anayosema ni ushindi wa nchi ya Tunisia, na inafungua ukurasa mpya wa kisiasa katika taifa hilo la Afrika Kaskazini.

Katiba iliyopitishwa inatoa fursa kwa rais kuwa na madaraka makubwa, kinyume na katiba iliyopita, ambayo madaraka hayo yaligawanywa na bunge.

Mwaka mmoja uliopita, rais Saied, alivunja serikali na kusitisha vikao vya  bunge katika kile kilichoonekana kama mapinduzi ya demokrasia nchini Tunisia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.