Nchi sita za Kiafrika kuzalisha chanjo ya mRNA
Nchi sita barani Afrika zimechaguliwa kuandaa uzalishaji wao wenyewe wa chanjo ya messenger RNA (mRNA), kama wanufaika wa kwanza wa mpango wa uzalishaji wa chanjo ya kimataifa wa shirika la Afya Duniani, WHO, shirika hilo limetangaza leo Ijumaa.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Afrika Kusini, Misri, Kenya, Nigeria, Senegal na Tunisia zimechaguliwa na shirika la Afya Duniani, WHO, kuruhusu bara la Afrika, ambalo lilipata nafasi ndogo ya kupata chanjo ya Covid-19, kutengeneza chanjo zake za kupambana na janga la Corona na magonjwa mengine.