Pata taarifa kuu
CAR-USALAMA

CAR: UN yafanya uchunguzi kuhusu mauaji yanayodaiwa kutekelezwa na vikosi vya jeshi

Umoja wa Mataifa unachunguza mauaji yanayodaiwa kufanywa karibu na mji wa Bria, nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, ambayo yalisabaisha vifo kadhaa wakati wa operesheni ya pamoja ya jeshi la Jmhuri ya Afrika ya Kati na mamluki wa kundi la Wagner kutoka Urusi kuanzia Januari 16 hadi 17, kwa mujibu wa vyanzo vya Umoja wa Mataifa.

Wanajeshi wa kigeni wakipiga doria katika mitaa ya Bria, mji unaokabiliwa na vitisho vya makundi yenye silaha katika Jamhuri ya Afrika ya Kati. (Picha ya kumbukumbu).
Wanajeshi wa kigeni wakipiga doria katika mitaa ya Bria, mji unaokabiliwa na vitisho vya makundi yenye silaha katika Jamhuri ya Afrika ya Kati. (Picha ya kumbukumbu). MIGUEL MEDINA / AFP
Matangazo ya kibiashara

Operesheni hii ililenga kundi la wapiganaji la Union for Peace in the Central African Republic (UPC), moja ya vyanzo hivi vimeliambia shirika la habari la AFP kwa sharti la kutotajwa jina.

"Zaidi ya raia 30 waliripotiwa kuuawa, wengine kwa risasi hewa," chama hiki kimeongeza, pia kikibainisha uwezekano wa kuwepo kwa visa vya uporaji ulivyotekelezwa na wahusika wa operesheni hiyo ya kijeshi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.