Pata taarifa kuu
SOMALIA

Aliyekuwa rais wa Somalia amtuhumu rais wa sasa kushambulia makazi yake

Rais wa zamani wa Somalia Hassan Sheikh Mohamoud amesema Jumapili kwamba wanajeshi walishambulia makazi yake na kwamba Rais Mohamed Abdullahi Mohamed ndiye aliyehusika na operesheni hiyo.

Afisa wa jeshi la Somalia anayeunga mkono viongozi wa upinzani wa Hawiye anatembea katika mitaa ya wilaya ya Yaqshid ya Mogadishu, Somalia Aprili 25, 2021.
Afisa wa jeshi la Somalia anayeunga mkono viongozi wa upinzani wa Hawiye anatembea katika mitaa ya wilaya ya Yaqshid ya Mogadishu, Somalia Aprili 25, 2021. REUTERS - FEISAL OMAR
Matangazo ya kibiashara

Kauli yake inakuja wakati makundi mawili ya wanajeshi walikabiliana kwa kurushiana risasi katika mji mkuu wa Mogadishu, ishara ya kuongezeka kwa mgawanyiko ndani yavikosi vya jeshi na usalama kati ya wafuasi wa rais wa sasa ambao walitaka aongezewe muhula wake na wale wanaopinga.

Kulingana na wadadisi, migawanyiko hii inaweza kuvuruga vikosi vya usalama vya Somalia kutoka kwenye vita vyao dhidi ya kundi la wanamgambo wa Kiislamu la al Shabaab, lenye mafungamano na al-Qaeda.

Rais Mohamed Abdullahi Mohamed alipitisha sheria katikati ya mwezi wa Aprili kuongeza muhula wake hadi miaka miwili, na kusababisha wimbi la upinzani nchini Somalia na kimataifa. Muhula wake wa miaka minne ulimalizika mwezi wa Februari mwaka huu bila mrithi yeyote kuteuliwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.