Ufaransa: Afisa wa polisi auawa kwa shambulio la kisu Rambouillet
Mtu mmoja alimdunga kisu afisa wa polisi mwanamke katika kituo cha polisi cha Rambouillet, kilomita 60 kutoka mji mkuu wa Ufaransa, Paris, kabla ya kuuawa kwa kupigwa risasi. Ofisi ya mashtaka inayopambana na ugaidi imeanzisha uchunguzi.
Imechapishwa:
Tukio hilo limetokea karibu saa 8:20 mchana kwenye katika kituo cha polisi cha Rambouillet. Mwanamume mmoja alimdunga kisu afisa wa polisi kwenye koo mara mbili alipokuwa akienda nyumbani kwa mapumziko ya chakula cha mchana. Chanzo cha polisi kinabaini kwamba muuaji alisema "Allah Akhbar" wakati wa kutekeleza uahlifu wake. Lakini alipigwa risasi na afisa mwingine wa polisi na kufariki dunia papo hapo.
Afisa huyo mwanamke aliyeuawa kwa shambulio la kisu alikua na umri wa miaka 49, na alikuwa afisa wa utawala wa sekretarieti ya kituo cha polisi cha Rambouillet. Afisa hyo wa polisi alikuwa mama wa watoto wawili, wa miaka 13 na 18.
Kitendo cha kinyama kwa shujaa wa kila siku
Mshambuliaji ni raia wa Tunisia mwenye umri wa miaka 36 ambaye aliwasili nchini Ufaransa mwaka 2009, akiingia kinyume cha sheria na tangu wakati huo aliishi nchini Ufaransa kwa vyeti halali. Hakujulikana na polisi na idara ya ujasusi, vyanzo kadhaa vya polisi vimethibitisha kwa shirika la habari la AFP. Kulingana na chanzo kilicho karibu na uchunguzi, alikuwa amehamia katika eneo la Rambouillet.
Waziri Mkuu Jean Castex na Waziri wa Mambo ya Ndani Gérald Darmanin wamezuru eneo la tukio. Katika ujumbe uliotumwa kwenye Twitter, kiongozi wa serikali ameshutumu "kitendo cha kinyama" dhidi ya "shujaa wa kila siku".
La République vient de perdre l’une de ses héroïnes du quotidien, dans un geste barbare et d’une infinie lâcheté.
— Jean Castex (@JeanCASTEX) April 23, 2021
À ses proches, je veux faire part du soutien de la Nation tout entière.
À nos forces de sécurité, je veux dire que je partage leur émotion et leur indignation.
"Hatutokubali kushindwa" kwa "ugaidi wa wa wanamgambo wa Kiislam," amesema Emmanuel Macron kwenye ukurasa wake wa Twitter.
Elle était policière. Stéphanie a été tuée dans son commissariat de Rambouillet, sur les terres déjà meurtries des Yvelines. La Nation est aux côtés de sa famille, de ses collègues et des forces de l’ordre. Du combat engagé contre le terrorisme islamiste, nous ne céderons rien.
— Emmanuel Macron (@EmmanuelMacron) April 23, 2021