Abiy Ahmed: "Hatutaki vita" na Sudan
Ethiopia "haitaki vita" na Sudan, Waziri Mkuu Abiy Ahmed amesema Jumanne wiki hii, wakati mvutano kati ya nchi hizo mbili uliendelea katika miezi ya hivi karibuni katika eneo la mpaka la Al-Fashaga.
Imechapishwa:
"Ethiopia·ina·matatizo·mengi,·na·hatuko·tayari·kupigana.·Hatuhitaji·vita.·Ni·bora·kusuluhisha·hilii·kwa·amani,"·Abiy·ameliambia·bunge.¶¶
"Hatutaki·vita,"·ameongeza,·huku·akiita·Sudan·jirani·"nchi·ndugu".¶¶
Mzozo·wa·mpakani·umekuwa·kati·ya·Sudan·na·Ethiopia·kwa·miongo·kadhaa·katika·eneo·kubwa·la·Al-Fashaga,·eneo·la·kilimo·la·hekta·milioni·1.2·ambapo·maeneo·ya·Amhara·na·Tigray·hukutana,·kaskazini·mwa·Ethiopia,·na·jimbo·la·Gedaref·mashariki·mwa·Sudan.¶¶
Kwa·zaidi·ya·miongo·miwili,·maelfu·ya·wakulima·wa·Ethiopia·wamekaa·katika·jimbo·hilo,·wakifanya·kilimo·na·kulipa·ushuru·kwa·jimbo·la·Ethiopia.¶¶
Kwa·miaka·mingi,·Khartoum·na·Addis·Ababa·wamefanya·mazungumzo·yenye·lengo·la·kuweka·wazi·mipaka,·bila·mafanikio.¶¶