Pata taarifa kuu
ETHIOPIA

Abiy Ahmed: "Hatutaki vita" na Sudan

Ethiopia "haitaki vita" na Sudan, Waziri Mkuu Abiy Ahmed amesema Jumanne wiki hii, wakati mvutano kati ya nchi hizo mbili uliendelea katika miezi ya hivi karibuni katika eneo la mpaka la Al-Fashaga.

Magari ya kijeshi ya Sudani yakitokea Khartoum kwenda Jimbo la Gedaref kwenye mpaka wa Ethiopia. Malori yaliyosheheni askari, silaha za kivita na magari ya kivita.
Magari ya kijeshi ya Sudani yakitokea Khartoum kwenda Jimbo la Gedaref kwenye mpaka wa Ethiopia. Malori yaliyosheheni askari, silaha za kivita na magari ya kivita. Nicolas Cortes - Nicolas Cortes
Matangazo ya kibiashara

"Ethiopia·ina·matatizo·mengi,·na·hatuko·tayari·kupigana.·Hatuhitaji·vita.·Ni·bora·kusuluhisha·hilii·kwa·amani,"·Abiy·ameliambia·bunge.¶¶

"Hatutaki·vita,"·ameongeza,·huku·akiita·Sudan·jirani·"nchi·ndugu".¶¶

Mzozo·wa·mpakani·umekuwa·kati·ya·Sudan·na·Ethiopia·kwa·miongo·kadhaa·katika·eneo·kubwa·la·Al-Fashaga,·eneo·la·kilimo·la·hekta·milioni·1.2·ambapo·maeneo·ya·Amhara·na·Tigray·hukutana,·kaskazini·mwa·Ethiopia,·na·jimbo·la·Gedaref·mashariki·mwa·Sudan.¶¶

Kwa·zaidi·ya·miongo·miwili,·maelfu·ya·wakulima·wa·Ethiopia·wamekaa·katika·jimbo·hilo,·wakifanya·kilimo·na·kulipa·ushuru·kwa·jimbo·la·Ethiopia.¶¶

Kwa·miaka·mingi,·Khartoum·na·Addis·Ababa·wamefanya·mazungumzo·yenye·lengo·la·kuweka·wazi·mipaka,·bila·mafanikio.¶¶

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.