Pata taarifa kuu
SUDAN-ETHIOPIA

Abdallah Hamdok na Abiy Ahmed waafikiana kuhusu mzozo wa Tigray

Baada ya mazungumzo kati ya Wazitri Mkuu wa SudanAbdallah Hamdok na mwenyeji wake wa Ethiopia, Jumapili Desemba 13, wawili hao wameafikiana kufanya mkutano wa dharura, utakaojumuisha mataifa yalio katika Jumuiya ya Maendeleo la Pembe ya Afrika IGAD, utakaohusu utatuzi wa mzozo wa Tigray.

Waziri mkuu wa Sudani, Abdallah Hamdock
Waziri mkuu wa Sudani, Abdallah Hamdock ASHRAF SHAZLY / AFP
Matangazo ya kibiashara

Abdallah Hamdok amekuwa kiongozi wa kwanza wa kigeni kuitembelea Ethiopia, tangu kuzuka kwa mapigano Novemba 4, ambayo yamezusha janga la kibinaadamu.

Ofisi ya Hamdok ilisema ziara hiyo inaongozwa na mazungumzo yenye tija na kwamba imekubaliwa kufanyika kwa mkutano wa dharura wa mataifa yalio katika Jumuiya ya Maendeleo la Pembe ya Afrika IGAD.

Hata hivyo ofisi ya waziri mkuu wa Ethiopia haijathibitisha tangazo la Waziri Mkuu wa Sudan, Abdallah Hamdok.

Wakati huo Taarifa iliyotolewa na ofisi ya waziri mkuu huyo wa Ethiopia inaeleza upande wa Sudan umeonesha uungaji mkono kwa serikali ya Ethiopia, katika jitihada zake za kusimamia utekelezwaji wa sheria za nchi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.