Kumi na Tisa wauawa katika shambulizi la watu wenye silaha Banyali Kilo, DRC
Watu 19 wameuawa na wengine kujeruhiwa baada ya kutokea kwa mashambulizi ya waasi ya hivi punde katika vijiji vitatu mkoani Ituri, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Imechapishwa:
Innocent Madukadala, kiongozi wa eneo la Banyali Kilo ambako mashambulizi hayo yalitekelezwa, anawashatumu waasi wa kundi la Codeco kuhusika katika mauaji hayo.
Kundi la Codeco limeendelea kunyooshewa kidole cha lawama kuhusima na vitendo vya ukatili ikiwa ni pamoja na mauaji, ubakaji na uporaji katika mkoa wa Ituri.
Shirika la Kimatiafa la kutatua migogoro la International Crisis Group katika ripoti yake mwezi uliopita, lilisema tangu mwaka 2017 utovu wa usalama katika mkoa wa Ituri, umesababisha vifo vya watu zaidi ya 1,000 na maelfu kuyakimbia makwao.