Serikali mpya ya DRC kutangazwa kati ya Agosti 19 na Septemba 7
Wananchi wa DRC watalazimika kuwa watulivu na kusubiri kidogo kabla ya kutangazwa baraza jipya la mawaziri katika utawala wa Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo, chanzo kilio karibu na ofisi ya rais kimesema.
Imechapishwa:
Serikali mpya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iliyokuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu inatarajiwa kutangazwa kati ya Agosti 19 na Septemba 7 mwaka huu, amesema Jeannine Mabunda, Spika wa Bunge la taifa.
Kwa ombi la Rais, Felix Tshisekedi, wabunge wameitishwa kushiriki katika kikao cha cha Jumatatu, Agosti 19 na watajadili kuhusu kuapisha mawaziri hao wapya.
Agosti 14, rais wa DRC alikataa kupitisha timu ya kwanza mawaziri, kwa sababu idadi ya wanawake na vijana haikuwa inatosha.