Pata taarifa kuu
TUNISIA-SIASA

Waziri Mkuu wa Tunisia kuwania kiti cha urais

Waziri Mkuu wa Tunisia na kiongozi wa chama cha Tahya Tounes Youssef Chahed, amewasilisha ombi la kuwania urais wakati wa uchaguzi utakaofanyika tarehe 15 mwezi ujao.

Waziri Mkuu wa Tunisia Youssef Chahed Novemba 8 Tunis, siku moja kabla ya ziara yake jijini Paris kuvutia wawekezaji wa kigeni kuja kuwekeza katika nchi yake.
Waziri Mkuu wa Tunisia Youssef Chahed Novemba 8 Tunis, siku moja kabla ya ziara yake jijini Paris kuvutia wawekezaji wa kigeni kuja kuwekeza katika nchi yake. FETHI BELAID / AFP
Matangazo ya kibiashara

Leo Ijumaa imekuwa ni siku ya mwisho kwa wanasiasa kuwasilusha maombi yao na hatua ya Chahed, inamweka katika nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huo.

Hata hivyo, anatarajiwa kupata ushindani kutoka kwa rais wa zamani Moncef Marzouki na Waziri wa Ulinzi Abdelkarim Zbidi.

Mshindi atamrithi rais wa zamani Beji Caid Essebsi, aliyefariki dunia mwezi uliopita akiwa na umru wa miaka 92.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.