Pata taarifa kuu
SOMALIA-AL SHABAB-USALAMA

Meya wa Mogadishu afariki dunia Doha, Qatar

Meya wa mji wa Mogadishu nchini Somalia, Abdirahman Omar Osman, amefariki dunia baada ya kujeruhiwa katika shambulio la kujitoa muhanga lililoua watu sita juma lililopita mjini Mogadishu. Amefariki dunia mjini Doha, Qatar, ambako alikuwa akipatiwa matibabu.

Mwakilishi Maalum mpya wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, James Swan (kushoto), akipokelewa na Meya wa Mogadishu Abdirahman Omar Osman (kulia) muda mfupi kabla ya shambulio dhidi ya ofisi ya Meya, Julai 24, 2019.
Mwakilishi Maalum mpya wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, James Swan (kushoto), akipokelewa na Meya wa Mogadishu Abdirahman Omar Osman (kulia) muda mfupi kabla ya shambulio dhidi ya ofisi ya Meya, Julai 24, 2019. UNSOM
Matangazo ya kibiashara

Abdirahman Omar Osman alijeruhiwa wakati shambulio la kujitoa mhanga katika ofisi yake walipokuwa katika mkutano wa masuala ya usalama.

Abdirahman Omar Osman ambaye aliishi katika mji wa London nchini Uingereza baada ya kuitoroka nchi yake kufuatia kuzuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe, alirejea nchini Somalia mwaka 2008 kusaidia kuijenga upya nchi yake inayoendelea kukumbwa na mdororo wa usalama.

Katika ukurasa wa twitter, ujumbe wa Marekani nchini Somalia umemtaja bwana Osman kuwa ''mshirika mzuri sana na aliyekuwa akiwatumikia raia wa Somalia bila kuchoka''.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.