Pata taarifa kuu
COMORO-SIASA-USALAMA

Ushindi wa Azali Assoumani wathibitishwa

Mahakama ya kikatiba nchini Comoro imethibitisha ushindi wa rais Azali Assoumani baada ya kupata asilimia 59 ya kura zote, katika uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi uliopita.

((Picha ya kumbukumbu) rais wa Comoro Azali Assoumani wakati wa kura ya maoni kuhusu marekebisho ya katiba, Moroni Julai 30, 2018.
((Picha ya kumbukumbu) rais wa Comoro Azali Assoumani wakati wa kura ya maoni kuhusu marekebisho ya katiba, Moroni Julai 30, 2018. TONY KARUMBA / AFP
Matangazo ya kibiashara

Hata hivyo, upinzani umekataa ushindi wake na kusema aliiba kura na hivyo hauwezi kumtambua kama rais wa Comoro.

Siku ya Jumanne rais Azali Assoumani amelihutubia taifa akiwa na ujumbe wa kujaribu kuwaunganisha wananchi wa taifa hilo, na kuwataka wapinzani kufungua ukurasa mpya na kukubali matokeo.

 

Upinzani chini ya vuguvugu la CNT ulikuwa umeahidi kuanzisha kampeni za vurugu nchini humo, huku waziri wa mambo ya ndani naye akiahidi kutekeleza sheria iwapo kutatokea vurugu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.