Wiki hii, Mahakama ya Kimataifa ya ICC imemhukumu mwaka mmoja, mwanasiasa wa upinzani nchini DRC Jean Pierre Bemba, baada ya kupatikana na kosa la kuwahonga mashahidi. Hata hivyo, hatafungwa jela kwa sababu tayari ameshakitumikia kifungo hicho. Je, hii inamaanisha nini kuelekea Uchaguzi Mkuu mwezi Desemba ? Tunathathmini na mchambuzi wetu Abdulkarim Atiki.