Pata taarifa kuu
CHINA-AFRIKA-USHIRIKIANO-UCHUMI

Cyril Ramaphosa: Hakuna ukoloni mamboleo katika misaada ya China

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amefutilia mbali kile anachoeleza "ukoloni mamboleo" kuhusu msaada wa China kwa Afrika. China imekua ikishtumiwa wakati mwingine kuongeza madeni kwa bara la Afrika.

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa anaongea katika majadiliano ya ngazi ya juu kati ya viongozi wa China na Afrika huko Beijing tarehe 3 Septemba 2018.
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa anaongea katika majadiliano ya ngazi ya juu kati ya viongozi wa China na Afrika huko Beijing tarehe 3 Septemba 2018. © AFP
Matangazo ya kibiashara

Katika kongamano la saba la kiuchumi kati ya China na Afrika Jumatattu wiki hii," Rais Ramaphosa almetetea uwepo wa China katika bara al Afrika, wakati Rais Xi Jinping akitangaza kutoa dola bilioni 60 kwa maendeleo ya Afrika.

Mkutano, ambao viongozi zaidi ya hamsini kutoka Afrika wanakutana na rais wa China, "unafutilia mbali hoja kwamba ukoloni mamboleo umewekwa barani Afrika, kama wanavyopenda kusema wapinzani," amesema Bw Ramaphosa.

Lakini neno "ukoloni mamboleo" lilizungumzwa hivi karibuni kuhusu mikopo mikubwa inayotolewa na Beijing kwa nchi zinazoendelea kwa miradi ya miundombinu. Mikopo hii inaweza kuwa na ugumu kwa kulipa, na hivyo kuongeza hatari kwa mkopo kwa nchi zinazonufaika.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.