Kesi ya aliyekuwa meya wa Dakar yaanza kusikilizwa
Kesi ya Rufaa inayomkabili aliyekuwa meya wa zamani wa jiji la Dakar nchini Senegal, Khalifa Sall itaanza kusikilizwa Jumatatu wiki hii baada ya kusimamishwa kwa muda wa mwezi mmoja kuruhusu upande wa utetezi kujiandaa.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Mahakama ya kwanza, Ilimhukumu meya huyo wa Dakar kifungo cha miaka 5 jela kufwatia kosa la Ubadhirifu na ufujaji wa fedha za serikali.
Khalifa Sall amkuwa akiitaja kesi hiyo kuwa ni ya kisiasa.
Nayo Jumuia ya ECOWASS ilitupilia mbali hukumu ya mahakama ya mwanzo ikisema kuwa haikuwa ya haki.
Wakili Démba Ciré Bathily, mmoja wa watetezi wake Khalifa Sall, amesema muda umefika kwa mteja wake kuachiliwa huru.