Korea Kusini yaionya DRC juu ya mashine za kupigia kura
Korea Kusini, siku ya Jumanne ilionya dhidi ya matumizi ya "mashine za kupigia kura" zinazotarajiwa kutumiwa wakati wa uchaguzi unaopangwa kufanyika nchini DRC mwishoni mwa mwaka huu.
Imechapishwa:
Mashine hizo zimetengenezwa na kampuni moja Huko Korea, huku ikisema kuwa inaogopa Kuwepo matokeo mabaya ya uchaguzi wa Desemba 23 ambao ndio utatatamtisha utawala wa Rais Joseph Kabila.
Kauli Hiyo imetolewa wakati kukiwa na tetesi kuwa kuna uwezekano wa kufanyika Udanganyifu ama wizi wa kura nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa faida ya vyama vinavyomuunga mkono rais Joseph kabila Kabange.
Seoul inaamini kuwa matumizi ya mashine hizi inaweza kusababisha machafuko zaidi nchini humo na kufanya kutoa matokeo yasiyo ya kweli, Taarifa kutoka Ubalozi wa Korea Kusini nchini DRC huko Kinshasa imesema.