Pata taarifa kuu
CONGO BRAZZAVILLE-VYOMBO VYA HABARI

Wanahabari wa RFI an AFP washambuliwa na polisi Brazzaville

Polisi waliokuwa wamevalia nguo za kiraia waliwavamia wanahabari waliokuwa wanakutana na Wakili wa mwanasiasa wa upinzani Andre Okombi Salissa nchini jijini Brazaville nchini Congo Brazaville.

Mji mkuu wa Congo, Brazzaville, ambako polisi imewavamia waandishi wa habari walipokua wakikutana na wakili wa upinzani..
Mji mkuu wa Congo, Brazzaville, ambako polisi imewavamia waandishi wa habari walipokua wakikutana na wakili wa upinzani.. Wikimedia/Jomako
Matangazo ya kibiashara

Ripota wa RFI na AFP Loïcia Martial amethibitisha kuvamiwa kwao, kabla ya mkutano huo kuanza.

Wanahabari hao walipigwa na kupokonywa vifaa vyao vya kazi.

Okombi ambaye alikuwa mpinzani wa rais Denis Sassou Ngueso wakati wa uchaguzi wa urais mwaka uliopita, anazuiliwa kwa madai ya kuhatarisha usalama wa nchi hiyo.

RFI na shirika la habari la AFP wanalaani kitendo hicho kiovu dhidi ya mwanahabari wao.

RFI na shirika la habari la AFP wanaomba wanahabari hao warudishiwe vifaa vyao vya kazi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.