TOGO-USALAMA-SIASA
Maandamano makubwa kufanyika Alhamii hii Togo
Upinzani nchini Togo, umetisha maandamani tena hii leo, baada ya hapo jana kufaanikisha maamndamano makubwa karibu nchi nzima, maandamano ambayo hata hjivyo yamegubikwa na vurugu katika baadhi ya maeneo ya nchi.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Waandamanaji wanamtaka rais wa nchi hiyo Faure Nyasingbe kuondoka madarakani.
Hatua hii inakuja baada ya upinzani kuomba mabadiliko ya katiba na kurejelea katiba ya mwaka 1992, huku ukitarajiwa kuandaliwa kura ya maoni, jambo ambalo limetupiliwa mbali na serikali.
Waziri wa usalama wa raia Yarke Damiane amesema waandamanaji wamesababisha hasara katika baadhi ya maeneo.