Pata taarifa kuu
ZAMBIA

Kiongozi wa upinzani nchini Zambia atimiza siku 100 jela

Kiongozi wa upinzani nchini Zambia Hakainde Hichilema ametimiza miaka 100 jela, baada ya kushtakiwa kwa makosa ya uhaini.

Hakainde Hichildma mgombea wa upinzani nchini Zambia
Hakainde Hichildma mgombea wa upinzani nchini Zambia REUTERS/Rogan Ward
Matangazo ya kibiashara

Hichilema amesema kwa kipindi chote hicho amekuwa akipitia kipindi kigumu kwa sababu haki zake msingi  zinakiukwa na amezuiwa katika mazingira mabaya.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, mwanasiasa huyo ameeleza kuwa pamoja naye, wafungwa wengine pia wanazuiwa katika mazingira yasiyo ya kuridhisha.

“Tunaamini kuwa licha ya makosa ambayo wafungwa hawa wamefanya, na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kuzuiwa kama mazingira haya mabaya,” ameandika.

“Wengine wetu bado, tunatafuta makosa tuliyofanya,” aliongeza.

Hichilema alikamatwa mapema mwaka huu baada ya msafara wake kuzuia msafara wa rais Edgar Lungu.

Mwanasiasa huyo ameyakanusha madai hayo na kusema ni ya kisiasa yanayotumiwa dhidi yake.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.