Pata taarifa kuu
JAMHURI YA AFRIKA YA KATI

Marekani yatangaza vikwazo dhidi ya viongozi wa makundi ya waasi wa Seleka na Anti Balaka

Marekani imetangaza vikwazo dhidi ya viongozi wawili wa makundi ya uasi nchini Jamhuri ya Afrika ya kati.

Waasi wa kundi  la Seleka wakiwa katika gariaina ya Pickup, kaskazini mwa mji wa Bangui, Januari 27 mwaka 2014.
Waasi wa kundi la Seleka wakiwa katika gariaina ya Pickup, kaskazini mwa mji wa Bangui, Januari 27 mwaka 2014. REUTERS/Siegfried Modola
Matangazo ya kibiashara

Washington DC inasema wawili hao ni  Abdoulaye Hissene anayeongoza kundi la lenye mrengo wa Kiislamu la Seleka na Maxime Mokom kiongozi wa kundi lenye mrengo wa Kikiristo Anti-Balaka.

Marekani inasema viongozi hao wameendelea kusababisha nchi ya Afrika ya Kati  kutokuwa na utulivu kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara.

Mali zao zimezuiliwa na Marekani lakini haijabainika ikiwa wana mali yoyote nje ya nchi.

Pamoja na hilo, raia wa Marekani wamepigwa marufuku ya kushirikiana na wawili hao kwa lolote.

Mzozo wa Jamhuri ya Afrika ya Kati ulianza mwaka 2012 baada ya waasi wa Seleka kumwondoa madarakani rais wa wakati huo Francois Bozize.

Watu zaidi ya elfu tano wamepoteza maisha na wengine zaidi ya 700,000 kuyakimbia makwao kwa muda miaka minne sasa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.