Pata taarifa kuu
ETHIOPIA-USALAMA

Maporomoko ya taka yagharimu maisha ya zaidi ya watu 30 Ethiopia

Zaidi ya watu 30 wamepoteza maisha kufuatia maporomoko ya taka kwenye eneo moja kubwa la kumwaga taka nje ya mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa.

Mlima mkubwa wa taka nchini Ethiopia, nje kidogo ya mji wa Addis Ababa, Machi 12, 2017.
Mlima mkubwa wa taka nchini Ethiopia, nje kidogo ya mji wa Addis Ababa, Machi 12, 2017. AFP
Matangazo ya kibiashara

Chanzo cha usalama kimesema kuwa watu kadhaa hawajulikani waliko tangu maporomoko hayo yatokee siku ya Jumamosi usiku.

Mashahidi wanasema kuwa watu zaidi ya 150 walikuwa eneo hilo, na inaminiwa kuwa wengi wao wamepoteza maisha.

Eneo hilo limekuwa likitumiwa kutupa taka kutoka kote mjini Addis Ababa kwa zaidi ya miongo mitano.

Inaarifiwa kuwa mabanda mengi ya watu yamefukiwa chini ya taka na watu wamekua wakitafuta vitu vyao.

Serikali nayo imekuwa ikijenga kiwanda cha kwanza barani Afrika, kwa lengo ya kuibadili taka hiyo kuwa nishati karibu na eneo hilo.

Sserikali ina mpango wa kuchoma taka na kuugeuza kuwa umeme. Hata hivyo wa eneo hilo wamekuwa wakisaka eneo hilo kujitafutia riziki.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.