Pata taarifa kuu
Mjadala wa Wiki

Wabunge nchini Rwanda kuidhinisha mabadiliko ya Katiba

Imechapishwa:

Katika makala hii tunazungumzia hatua ya Wabunge nchini Rwanda kupitisha muswada utakaoidhinisha kubadilishwa kwa vipengee vya katiba vitakavyoruhusu rais Paul Kagame kuongoza kwa muhula wa tatu.Katika bunge lililokuwa limejaa wabunge na wananchi waliofurika kushuhudia mjadala huo bungeni, walishangilia na kulitaja jina la rais Kagame baada ya wabunge wote katika baraza la seneti na bunge kupitisha muswada huo kama hatua ya mwanzo kuelekea kufanyika mabadiliko ya katiba.Katika kipindi cha miezi kadhaa iliyopita mamilioni ya raia nchini Rwanda wamekuwa wakitia sahihi pendekezo la kumtaka rais Kagame kuendelea kuongoza taifa hilo hata baada ya kukamilika kwa muhula wake wa pili.

Studi RFI Kiswahili jijini Dar es Salaam
Studi RFI Kiswahili jijini Dar es Salaam RFI/BILALI
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.