Pata taarifa kuu
AU-BURUNDI-LIBYA-USALAMA-SIASA

Mzozo wa Burundi na Libya katika mkutano wa AU

Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika linakutana kwa muda wa siku mbili tangu leo Jumamosi mjini Johannesburg, nchini Afrika Kusini.

Mkutano wa kilele wa marais wa nchi kutoka bara la Afrika unaanza Jumapili, lakini marais hao wameanza kuwasili Jumamosi Juni 13 jijini Johannesburg.
Mkutano wa kilele wa marais wa nchi kutoka bara la Afrika unaanza Jumapili, lakini marais hao wameanza kuwasili Jumamosi Juni 13 jijini Johannesburg. REUTERS/Siphiwe Sibeko
Matangazo ya kibiashara

Kwenye ajenda ya mkutano wa marais kabla ya ufunguzi rasmi wa mkutano huo Jumapili, masuala kadhaa yatazungumziwa kama mzozo wa kisiasa Burundi, kuongezeka kwa makundu ya kigaidi barani Afrika au mgogoro wa Sudan Kusini.

Lakini pia litazungumziwa katika mkutano huo suala tata la vijana wengi kutoka barani wanaoelekea Ulaya wakipitia katika bahari ya ambapo wamekua vijana wengi wamepoteza maisha kutokana na kuzama kwa boti wanazotomia katika safari hizo za majini.

Mkutano huo wa viongozi wa nchi kutoka bara la Afrika unaoanza kesho jumapili pia utajadili juu ya mgogoro unaolikumba taifa la Sudan Kusini lakini pia mikakati ya pamoja katika kuimarisha pambano dhidi ya ugaidi barani Afrika.

Msemaji wa Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi hata hivyo amesema kiongozi huyo hatahudhuria mkutano huo.

Leo Jumamosi na Jumapili, suala litakalojadiliwa kwa upana ni namna ya kutuliza machafuko yanayoendelea nchini Burundi kutokana na hatua ya rais Pierre Nkurunziza kutangaza kuwa atawania urais kwa muhula wa wa tatu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.