Pata taarifa kuu
RWANDA-FDLR-DRC-UN-USALAMA

Muda uliotolewa kwa waasi wa FDLR wamalizika

Januari 2 ni siku ya mwisho kwa muda uliyotolewa kwa waasi wa Kihutu wa Rwanda wa FDLR kuwa wawe wameshajisalimisha na kuweka silaha chini.

Kundi la wapiganaji wa FDLR, nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo (picha ya zamani).
Kundi la wapiganaji wa FDLR, nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo (picha ya zamani). Reuters
Matangazo ya kibiashara

Jumuiya za kikanda, ICGLR na SADC, zikiungwa mkono na jumuiya ya kimataifa yalikuwa yametoa siku ya leo kuwa siku ya mwisho kwa waasi wa kundi la FDLR kuwa wameshajisalimisha kwa hiari yao na kukubali kupelekwa katika kambi iliyojengwa kwa minajili ya kurejeshwa katika maisha ya kiraia.

Silaha ambazo zilisalimishwa na waasi wa FDLR, nyuma wanaonekana vijana wa kundi hilo waliojisalimisha
Silaha ambazo zilisalimishwa na waasi wa FDLR, nyuma wanaonekana vijana wa kundi hilo waliojisalimisha MONUSCO

Kwa wale wote ambao watakua bado kujiunga na wengine katika mpango huo watalazimika kupokonywa silaha zao kwa nguvu katika operesheni ya pamoja ya kijeshi itakayoendeshwa na jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na kikosi cha wanajeshi wa Umoja wa Mataifa nchini Congo Monusco.

Wanamgambo wa FDLR wajisalimisha katika kijiji cha Kateku mashariki mwa DRC, Mei 30 mwaka 2014.
Wanamgambo wa FDLR wajisalimisha katika kijiji cha Kateku mashariki mwa DRC, Mei 30 mwaka 2014. REUTERS/Kenny Katombe

Wapiganaji 400 kwa jumla ya wapiganaji walio kati ya 1500 na 3000, kulingana na takwimu, ndio wameshajiunga na mpango huo, katika kambi iliyojengwa na Monusco.

Kwa upande wake kundi la waasi wa Kihutu wa Rwanda la FDLR limebaini kwamba operesheni hizo hazina maana yoyote na zina lengo tu ya kumwaga damu ya raia wasio na hatia, ikiwa ni pamoja na wapiganaji waliopokonywa silaha pamoja na raia wa kawaida wanaishi pamoja nao.

" Jumuiya ya kimataifa ina kosa kwa sababu imekataa kutekeleza ombi letu kwa kuishinikiza serikali ya Rwanda kufungua nafasi kwa wanasiasa na kuhakikisha haki na uhuru wa wananchi wake", msemaji wa FDLR, La Forge Bazeye Fils ameiambia RFI.

Waasi wa Kihutu wa Rwanda wa FDLR, kilomita 150 kaskazini mashariki mwa Goma, mwaka 2009.
Waasi wa Kihutu wa Rwanda wa FDLR, kilomita 150 kaskazini mashariki mwa Goma, mwaka 2009. AFP/ Lionel Healing

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.