Pata taarifa kuu
TUNISIA

Maandamano ya kuipinga serikali ya kiislamu nchini Tunisia yazidi kushika kasi

Polisi nchini Tunisia wamelazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya maelfu ya waandamnaji katika barabara za mji wa Sidi Bouzid wanaondamana kutaka serikali ya Kislamu kuondoka madarakani. Waandamanaji hao wameendelea kupaza sauti zao kwa zaidi ya juma moja sasa baada ya kuuawa kwa kiongozi wa upinzani Mohammed Brahmi.

REUTERS/Anis Mili
Matangazo ya kibiashara

Wafanyakazi waliokuwa wanakwenda kazini siku ya jumatatu walizuiliwa kuingia sehemu zao za kazi na waandamanaji hao waliowataka kujiunga nao ili kuendelea kushinikiza chama cha Ennahda kuondoka madarakani.

Wakati makabiliano hayo yakiendelea, viongozi wa serikali wamekuwa wakikutana kwa dharura kujadili mustakabali wa maandamano hayo ambayo yanayofiwa huenda yakawa makubwa kama yale yaliyoingusha serikali ya Rais wa zamani Zine El Abidine Ben Ali.

Mohammed Brahmi anakuwa kiongozi wa pili wa upinzani nchini humo kuuawa baada ya kiongozi mwingine Chokri Belaid kupigwa risaisi na kuuawa nyumbani kwake mapema mwaka huu.

Upinzani nchini Tunisia umeendelea kuitumu serikali kwa kuwauawa viongozi wao tuhma ambazo serikali imeendelea kukanusha.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.