GUINEA BISSAU
Kiongozi wa kijeshi anayetuhumiwa kufanya jaribio la kupindua serikali ya Guinea Bissau akamatwa
Kapteni wa jeshi anayekabiliwa kesi ya kujaribu kufanya mapinduzi ya kijeshi nchini Guinea ya Bissau amekamatwa,taarifa za jeshi la nchi hiyo zimebainisha.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kapteni Pansau N'Tchama anatuhumiwa kusimamia shambulizi la juma lililopita ambalo lilisababisha vifo vya watu 6.
Jeshi nchini humo lilidhibiti serikali katika kipindi cha uchaguzi wa uraisi mnamo mwezi April.
Serikali ya mpito nchini humo ambayo iliteuliwa na jeshi imeituhumu wakoloni wa kireno waliotawala zamani kuhusika na mashambulizi dhidi ya nchi hiyo.