Pata taarifa kuu
ZIMBABWE-MUGABE-SIASA-UCHUMI

Mugabe aendelea kutazamwa kama mtu muhimu kwa Zimbabwe

Gazeti la serikali nchini Zimbabwe limeripoti kuwa, rais wa zamani Robert Mugabe atapewa makazi, gari na ndege ya kibinafasi na serikali kama malipo ya uzeeni.

29 juin 2008. Robert Mugabe est réélu pour un sixième mandat dans un climat tendu et fait face aux critiques internationales.
29 juin 2008. Robert Mugabe est réélu pour un sixième mandat dans un climat tendu et fait face aux critiques internationales. AFP PHOTO / Alexander Joe
Matangazo ya kibiashara

Pamoja na hayo atawepewa walinzi sita wa kibinafsi pamoja na wafanyikazi 20.

Haya n baadhi ya masharti ambayo yalirahisisha kukubali kujizulu kwa Mugabe mwenye umri wa miaka 93, mwezi uliopita.

Hayo yanajiri wakati ambapo maafisa wa ngazi ya juu katika jeshi waliomtimua madarakani Robert Mugabe wameteuliwa kwenye nafasi muhumu serikalini.

Rais mpya ya Zimbabwe Emmerson Mnangagwa aliwateua makamu wake wawili. Jenerali Constantino Chiwenga na Waziri wa zamani Kembo Mohadi wote waliapishwa siku ya Alhamisi asubuhi.

Jenerali Constantino Chiwenga aliongoza jeshi kumtimua mamlakani aliyekuwa rais wa taifa hilo Robert Mugabe mnamo mwezi Novemba.

Alistaafu hivi karibuni na kuwa naibu kiongozi wa chama tawala cha Zanu-PF mnamo Disemba 2.

Rais mpya Emmerson Mnangagwa alichukua hatamu ya uongozi baada ya jeshi kuingilia kati tarehe 15 mwezi Novemba kufuatia mgogoro wa kumrithi Robert Mugabe.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.