Pata taarifa kuu
CECAFA-MICHEZO-SOKA

Michuano ya CECAFA kwa wanawake yaendelea, Kenya yasaka ushindi wa pili

Kenya inatafuta ushindi wake wa pili katika michuano ya soka kwa wanawake kuwania taji la Afrika Mashariki na Kati CECAFA, inayoendelea jijini Dar es salaam nchini Tanzania.

Timu ya taifa ya soka ya wanawake Harambee Starlets
Timu ya taifa ya soka ya wanawake Harambee Starlets Harambee Starlets/Twitter.com
Matangazo ya kibiashara

Harambee Starlets itamenyana na Djibouti, huku Ethiopia ikimenyana na Uganda.

Siku ya Jumatatu, Sudan Kusini iliishinda Zanzibar mabao 5-0, huku Tanzania ikiwaangusha Burundi mabao 4-0.

Sudan Kusini nayo itamenyana na Burundi siku ya Jumatano kutafuta ushindi wake wa pili, huku Zanzibar ikimenyana na Tanzania bara.

Uganda na Kenya zote zina alama tatu, huku Tanzania ikiongoza kundi la B kwa alama 6 baada ya kushinda mechi zake mbili.

Burundi na Sudan Kusini baada ya kupata ushndi wa kwanza, zina alama tatu.

Matokeo yaliyopita:-

Burundi 5-0 Zanzibar

Kenya 0-2 Ethiopia

Sudan Kusini 5-0 Djibouti

Tanzania 9-0 Sudan Kusini

Uganda 13-0 Djibouti

Tanzania 4-0 Burundi

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.