Michuano ya Vijana barani Afrika yaanza nchini Misri
Makala ya tatu ya mchezo wa soka, kutafuta bingwa wa Afrika kwa wachezaji wasiozidi miaka 23, inaanza kutifua vumbi nchini Misri, siku ya Ijumaa.
Imechapishwa:
Michuano hii, inatarajiwa kumalizika tarehe 22 mwezi Novemba.
Timu zitakazomaliza katika nafasi tatu bora, zitafuzu katika michezo ya Olimpiki itakayofanyika mwaka 2020 jijini Tokyo nchini Japan.
Nigeria ndio mabingwa watetezi wa taji hili. Mwaka 2015, michuano hii ilifanyika jijini Dakar nchini Senegal.
Mataifa yanayoshiriki ni pamoja na wenyeji Misri, Cameroon, Ghana, Ivory Coast, Mali, Nigeria, Afrika Kusini na Zambia.
Makundi:
Kundi la A : Misri, Mali, Cameroon na Ghana
Kundi B: Nigeria, Ivory Coast, Afrika Kusini na Zambia.
Ratiba ya Ijumaa
Misri vs Mali
Cameroon vs Ghana
Ratiba ya Jumamosi
Nigeria vs Ivory Coast
Afrika Kusini vs Zambia