TANZANIA-AFRIKA-SOKA
Afrika U-17: Timu nne kusaka tiketi ya nusu fainali
Mechi za nusu fainali kuwania taji la bara Afrika kwa wachezaji wasiozidi miaka 17, zitachezwa siku ya Jumatano wiki hii. Timu nne zitashiriki michuano hiyo ikiwa ni pamoja na Nigeria, Guinea, Angola na Cameroon.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mechi zote zitachezwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam nchini Tanzania.
Nigeria watakuwa wa kwanza, kumenyana na Guinea kuanzia saa 10 jioni lakini baadaye Cameroon watamenyana na Angola kuanzia saa moja na nusu.
Fainali itachezwa siku ya Jumapili.
Mataifa haya manne, Nigeria, Guinea, Cameroon na Angola, zote zimefuzu katika fainali ya kombe la dunia kwa vijana utakayofanyika mwezi Oktoba nchini Brazili.